Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) Dkt .Tumaini Gurumo na Mwakilishi wa Chuo cha Korea Institute of Maritime and Fisheries Technology (KIMFT) Dkt. Min Jung (kulia) wakionyesha nyaraka ya Mkataba wa Makubaliano walioyaingia katika kubadilishana uzoefu kati ya vyuo hivyo.
Mhandisi Mkuu wa Meli na Mkufunzi wa DMI, Deism Mlay akitoa ufafanuzi wa elimu na mafunzo yanayotolewa chuoni kwa wanafunzi katika maonesho ya Elimu ya Vyuo Vikuu Pemba 2023.
Mkuu wa Chuo cha Bahari DMI, Dk. Tumaini Gurumo (Katikati) pamoja na Makamu Wakuu wa chuo wakiushukuru Ugeni wa Balozi wa Korea nchini Tanzania.
Mtaalamu kutoka DMI Bi. Beatrice Nyagusi akitoa maelezo juu ya elimu na mafunzo yanayotolewa chuoni kwa wageni waliotembelea banda la DMI katika maonesho ya TCU 2023.
Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Suleiman Makame (MP) wa nne kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Chuo, wageni waalikwa na wanakamati wa kongamano la pili la uchumi wa Buluu lililofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa JNICC.
Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Suleiman Makame akihutubia washiriki wa kongamano la pili la uchumi wa buluu lililofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa JNICC
Kuwa taasisi bora katika mafunzo, utafiti na ushauri katika taaluma za baharini na zinazohusiana
Dira
Kutoa mafunzo ya hali ya juu yanayo endeshwa na mahitaji, utafiti na huduma za ushauri katika taaluma za baharini na taaluma zinazo husiana katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara na kwingineko